Jumatatu, 13 Juni 2016

MATUMIZI YA NETI TU HAYATOSHI KUZUIA MALARIA

MATUMIZI YA NETI TU HAYATOSHI KUZUIA MALARIA
Ushawahi kujiuliza ni kwa nini unaweza ukawa unalala kwenye neti kila siku lakini bado ukapata malaria? 
Na kuna watu wengi ambao wamepata malaria hali ya kuwa wanalala ndani ya chandarua kila siku? 
Sababu ni rahisi sana. KUNG'ATWA NA MBU UKIWA NJE YA NETI. HUSUSAN KABLA YA KULALA KITANDANI
Muda wa kuanzia saa 12 jioni mpaka saa 4 usiku watu wengi hung'atwa na mbu na kuweza kupata malaria. Huu ndo ule wakati wa maongezi ya jioni nje, ukumbini au chumbani; kuangalia televisheni sebuleni, kuwa karibu na bustani ukipata chakula na vinywaji, umepumzika sebuleni au chumbani na kadhalika. Mara nyingi tunakuwa nje ya chandarua muda huo na huweza KUNG'ATWA na mbu.
JINSI YA KUJIKINGA
Wakati upo nje ya neti jikinge dhidi ya kung'atwa na mbu kwa kufanya yafuatayo :
1. Vaa nguo zinazofunika mwili wako wote





Hapa unashauriwa kuvaa suruali na mashati ya mikono mirefu, gauni refu na lenye mikono mirefu, soksi zisizoweza kupenyezwa na mdomo wa mbu nk
2. Paka dawa ya kuzuia mbu wasikung'ate wala kutua mwilini mwako
Kwa Kiingereza ndizo huitwa "mosquito repellents". Hizi husaidia kufukuza na kuwazuia mbu wasikung'ate kabisa

3. Tumia dawa za kuzuia malaria
Hususan kama unatoka sehemu ambayo haina malaria kwa wingi kwenda sehemu yenye tatizo kubwa la malaria. Pata ushauri wa daktari ili kufanikisha jili
4. Hakikisha usafi wa mazingira na kutokomeza mazalia ya mbu
Haya hujumuisha madimbwi ya maji, vichaka nk



5. Epuka maeneo yenye mbu muda wa jioni
Inawezekana ukawa upo mbali na nyumbani au ukashindwa kufanya mambo ya hapo juu. Hapa cha msingi jiepushe na maeneo yenye mbu, kama vile yaliyo na giza na yaliyopo karibu na mazalia ya mbu.
MALARIA INAZUILIKA. TUANZE SASA.......





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni