Jumatatu, 13 Juni 2016

MAFUTA NA LOSHENI SAHIHI KWA NGOZI YAKO

MAFUTA NA LOSHENI SAHIHI KWA NGOZI YAKO
Kama mnavyojua ngozi zetu zinatofautiana. Kuna watu wenye ngozi kavu, kuna wenye ngozi za mafuta, kuna wenye ngozi za kawaida (sio kavu wala sio za mafuta) na wenye ngozi mchanganyiko.
Kwa upande wa mafuta na losheni pia kuna mafuta na losheni kwa ajili ya ngozi kavu, kuna ya ngozi za kawaida, kuna ya ngozi mchanganyiko na ya ngozi za mafuta.
Bahati mbaya ni kwamba vipodozi vingi vinatoka nje, na vimeandikwa kwa lugha ya Kiingereza. Sasa cha msingi ni kujua aina ya ngozi yako kwanza na kisha kuchagua mafuta na losheni inayofaa kwa ngozi yako.
Pima ngozi yako sasa. Unaweza kufanya hivi hospitali, maduka ya urembo na Vipodozi nk
Pia S&E HEALTH SOLUTIONS vipimo vyake vinapatikana na unaweza kutumiwa popote Tanzania.
Baada ya kujua aina ya ngozi yako sasa nunua na tumia mafuta au losheni inayoendana nayo.
1. Kama ngozi yako ni kavu tumia losheni iliyoandikwa FOR DRY SKIN
2. Kama ngozi yako ni ya mafuta tumia losheni iliyoandikwa FOR OILY SKIN
3. Kama ngozi yako ni ya kawaida tumia losheni iliyoandikwa FOR NORMAL SKIN
4. Kama ngozi yako ni mchanganyiko tumia losheni iliyoandikwa FOR COMBINATION SKIN

Pia kuna mafuta na losheni ambayo yanafaa kwa aina zote za ngozi. Haya huweza kutumiwa na mtu mwenye ngozi ya aina yoyote. Yenyewe utakuta imeandikwa FOR ALL SKIN TYPES.

Mafuta na losheni zinazoendana na aina ya ngozi yako ndiyo vitakupa matokeo mazuri bila kuathiri ngozi yako kama vile kukuletea chunusi, jasho jingi nk
S&E HEALTH SOLUTIONS inakutakia kila la kheri katika kuboresha afya na uzuri wako!


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni