Alhamisi, 23 Juni 2016

MAMBO (YA KITABIA) YANAYOKUWEKA KATIKA HATARI YA KUPATA KISUKARI

Ugonjwa wa kisukari huweza kusababishwa au kuchangiwa na mambo mbalimbali ya ndani na nje ya mwili. Mengine tuna uwezo wa kuyaratibu na kurekebisha sisi wenyewe tena kwa urahisi tu.

Miongoni mwa mambo hayo ni
1. Kukosa mazoezi au kufanya mazoezi kidogo sana
2. Uvutaji wa sigara













3. Msongo
4. Kulala sana au kutolala vya kutosha
Kwa bahati nzuri hayo mambo yote ni ya kitabia na unaweza kuyarekebisha. Unaweza ukajilinda dhidi ya kisukari kwa
i. Kupunguza uzito na mwili wenye afya nzuri
ii. Kujishughulisha kwa mambo mbalimbali kama vile kazi zinazotumia nguvu, misuli na mazoezi 
iii. Kula vizuri
Epuka kula kwa wingi vyakula vya wanga, sukari, mafuta na nyama nyekundu na za kupakiwa kiwandani
iv. Acha kuvuta sigara
Ukizingatia hayo utakuwa umejiepusha kupata kisukari au itakusaidia sana kuwa na afya nzuri hata kama una kisukari

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni