Jumatano, 27 Aprili 2016

TATIZO LA MAFUTA MENGI USONI
Habari rafiki! Karibu leo tuzungumzie tatizo la mafuta mengi usoni.
Mafuta ni moja kati ya vitu muhimu sana katika ngozi zetu. Na chini ya ngozi zetu (ndani ya mwili) kuna mafuta mengi yamehifadhiwa na pia kuna seli ambazo kazi yake kubwa ni kutoa haya mafuta. Mafuta haya yana kazi kuu kama mbili hivi:
Kwanza ni kutusaidia wakati wa baridi. Yanazuia joto kupotea na hutumika kuongeza joto la mwili
Pili yanasaidia kuipakaa ngozi na kuikinga dhidi ya maji kupotea na ngozi kusinyaa au kukauka. Kwa maana hii mafuta husaidia kuzifanya ngozi zetu kuwa nzuri na afya nzuri. Ngozi yenye mafuta mengi huwa na faida ya kutowahi kuzeeka, kutokauka, kutopata maambukizi kiurahisi na kutohitaji mafuta mengi ya kuongezea kwa ajili ya kuitunza.
TATIZO LA MAFUTA MENGI



Mafuta yakiwa ya wastani maisha yanakuwa mazuri pia na ngozi inaweza kukubali vipodozi mbalimbali vya kuongezea uzuri na urembo wa ngozi.
Mafuta yakiwa mengi yanaweza kushindwa kutoka vizuri wakati wa kuletwa nje ya ngozi na hivyo kukwama kutokana na kuzibwa kwa ngozi na uchafu au seli zilizokufa, matokeo yake ni kumletea mtu chunusi. Mara nyingi watu wenye mafuta mengi usoni wanakabiliwa na tatizo la chunusi na upele mwingine.
Inawezekana mtu akawa na asili tu ya kuwa na mafuta mengi, au yakaanza kuzalishwa kwa wingi kutokana na vipodozi anavyotumia kama vile scrub na vipodozi vingine ambavyo vitaifanya ngozi ihisi mafuta yamepungua kwenye uso wa ngozi na hivyo kuanza kuzalisha na kutoa mafuta mengi zaidi kuja nje ya ngozi.
USHAURI NA KUKABILIANA NA TATIZO LA MAFUTA MENGI USONI
Kama una mafuta mengi usoni ni faida sana kwako, kwa kuwa ngozi yenye mafuta mengi huwa na faida ya kutowahi kuzeeka, kutokauka, kutopata maambukizi kiurahisi na kutohitaji mafuta mengi ya kuongezea kwa ajili ya kuitunza.
Kama yanakusumbua kwa kujaa zaidi, kukuletea chunusi na matatizo mengine basi unaweza kuwa unayaosha kwa maji au kuyafuta kwa kitambaa kisafi na laini.
Kwa upande wa ushauri,
Kwanza tumia vipodozi (Lotion, Cream na Mafuta) ambavyo ni maalum kwa ajili ya ngozi za mafuta. Mara nyingi utakuta vimeandikwa FOR OILY SKIN au KWA NGOZI YA MAFUTA




Pili epuka scrub au itumie kwa ufundi ili isikusababishie mafuta mengi zaidi kuzalishwa na kukuzidishia chunusi. Hakikisha unapaka moisturiser nzuri kila baada ya kuscrub ili kuifanya ngozi yako isihisi ukavu na isizalishe mafuta mengine mengi zaidi
Tatu unaweza ukatumia poda na sabuni zinazosaidia kupunguza mafuta usoni. Mifano ni poda ya POND'S ile iliyoandikwa OIL CONTROL na sabuni za DOVE na PEARS zilizoandikwa OIL CONTROL SOAP

Nne usipasue chunusi yoyote kama nazo zitakuwepo. Kupasua chunusi kutakuachia makovu na madoa madogo madogo ambayo yatakuharibia uso wako.

Tano unashauriwa kutumia facial cleanser/face wash ili kuweza kuondoa uchafu, seli zilizokufa na mafuta yaliyoziba matundu.
Usifadhaike na ngozi yenye mafuta, ni nzuri. Ishi nayo vizuri.
Pia unaweza kuonana au kuwasiliana na wataalam na washauri wa afya, uzuri na vipodozi kwa ushauri na maelezo zaidi
S&E BEAUTY SOLUTIONS
WATAALAM NA WASHAURI WA AFYA, UREMBO NA VIPODOZI
0 659 528 724 au 0 784 082 847
Facebook : S&E BEAUTY SOLUTIONS

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni