Jumapili, 24 Aprili 2016

KUJIPENDEZESHA SAWA, KUJIHARIBU HAPANA!

  KUJIPENDEZESHA SAWA, KUJIHARIBU HAPANA !

Unaendeleaje rafiki? Karibu kwenye somo la leo la kukushauri kujipendezesha na kukushauri kutokujiharibu kwa kupitia vipodozi unavyotumia.
Ni haki na ni vizuri kujipendezesha na kuwa na muonekano mzuri kwani muonekano wako ni sehemu ya moyo na maisha yako. Ukiwa na muonekano mzuri utachukuliwa kama ni mtu wa kuheshimiwa, kupendwa na kuthaminiwa. Ukiwa na muonekano mbaya inakuwa kinyume chake, labda uwe na vitu vingine vya kipekee sana.

VIPODOZI VYA KUTUMIA ILI KUJIPENDEZESHA VIZURI
Ukitaka kujipendezesha vizuri unashauriwa kuujua vizuri mwili wako (ngozi, kucha, nywele nk) ili utumie vipodozi vinavyoendana nao na malengo yako
Kama ni ngozi ni lazima ujue aina ya ngozi yako (Ngozi kavu, Ngozi ya mafuta, Ngozi ya kawaida au Ngozi mchanganyiko) ili utumie bidhaa zinazoendana na ngozi yako
Pia chagua maduka ya kuaminika kwa ajili ya kupata vipodozi vyako. Maduka mengine wanakuwa wanauza na vipodozi feki, visivyosajiliwa, vyenye sumu, vilivyopigwa marufuku, vilivyoharibika au kupita muda wake wa matumizi na kadhalika. Epuka sana kutumia vipodozi hivyo na hata kununua vipodozi kutoka kwenye maduka hayo
Chagua vipodozi vyenye ubora mzuri na ufanisi mzuri na vinavyopatikana kwa bei unayoimudu ili uweze kuvitumia vizuri na kwa uhuru bila kuathiri uchumi wako
Pata ushauri wa kitaalam kabla ya kuanza kutumia vipodozi usivyovijua. Mwambie unachohitaji kwenye mwili wako ili yeye akushauri vipodozi vya kutumia

VIPODOZI VITAKAVYOHARIBU MWILI WAKO



Usipotumia vipodozi vizuri unaweza ukapata madhara mengi na makubwa. Machache kati ya hayo ni kansa ya ngozi, maini, ubongo, mapafu na mfumo wa damu; ngozi kuungua, ngozi kuwasha sana, upofu, upotevu wa fahamu wa mara kwa mara, uziwi, kuumwa kichwa, kizunguzungu, fangasi na magonjwa mengine kwenye ngozi, aleji (mzio) ya ngozi, kuchubuka kwa ngozi, mabaka mabaka, chunusi kubwa kubwa, ngozi kuwa nyembemba sana na laini kiasi cha kidonda kuchelewa au kushindwa kupona endapo utapata jeraha au kufanyiwa operesheni na mengineyo mengi.
Vipodozi vitakavyokuharibu ni vile ambavyo
i.                    Haviendani na ngozi au mwili wako
Kwa mfano mtu mwenye uso au ngozi ya mafuta akitumia kipodozi kwa ajili ya ngozi kavu basi inaweza kumletea chunusi nyingi na matatizo mengine. Usitumie kipodozi chochote ambacho sio kwa ajili ya aina ya ngozi au mwili wako
ii.                  Vina kemikali ambazo ni sumu na hudhuru mwili wa binadamu na viungo vyake
Mifano ni Mercury (Zebaki), Hydroquinone na Betamethasone
iii.                Vimeharibika au muda wake wa matumizi umeisha. Hivi vinakuwa havina garantii ya ubora, ufanisi wala usalama
Hivi navyo ni hatari kwa afya yako, usivitumie.
iv.                Vipodozi ambavyo vimepigwa marufuku, havijaidhinishwa na kusajiliwa na Mamlaka Ya Chakula Na Dawa Tanzania (TFDA)
Hivi navyo havina garantii ya ubora, ufanisi wala usalama. Usivitumie.
v.                  Matumizi yake hayaendani na mahitaji yako
Ni vyema kuvielewa vizuri vipodozi au kupata ushauri wa vipodozi vya kutumia kulingana na matatizo au mahitaji yako. Usitumie vipodozi ambavyo haviendani na tatizo au hitaji lako, maana utakosa matokeo unayoyahitaji, utapoteza pesa, muda na vinaweza kukuletea matatizo mengine ambayo haukuwa nayo.

KUJIPENDEZESHA SAWA, KUJIHARIBU HAPANA!
Tunakushauri usitumie kipodozi chochote ambacho sio salama hata kama kinakuletea matokeo mazuri kwa haraka. Matatizo mengi ya vipodozi visivyo salama huwa ni makubwa na hayatibiki kirahisi, na mengine yanaua au kukupa ulemavu wa kudumu. Yanaweza kuja haraka au pole pole, kwa hiyo hata kama hauyaoini kwa sasa basi baadae yatafika.
Furahia ujana, furahia uzee. Vipodozi vibaya vinaweza vikakuzeesha haraka na kukupa matatizo mengi sana baadae na uzeeni.
Onana na wataalam wa urembo na vipodozi, pata ushauri.
Kwa maelezo zaidi na ushauri juu ya vipodozi na kupendezesha mwili wako wasiliana na wataalam

Ujumbe huu umeletwa kwako na wataalam na washauri wa Afya, Urembo na Vipodozi
S&E BEAUTY SOLUTIONS
TEMEKE BUZA NA ILALA BUNGONI
DAR ES SALAAM
Simu : 0 659 528 724 au 0 784 082 847

Kurasa za Facebook :          S&E BEAUTY SOLUTIONS
                          Na                 MSHAURI WA AFYA
                                  





                                  KUJIPENDEZESHA SAWA, KUJIHARIBU HAPANA !

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni