Jumatatu, 2 Mei 2016

DALILI ZA MAGONJWA HUWEZA KUFANANA. PATA UHAKIKA KUTOKA KWA WATAALAM
Dalili za ugonjwa mmoja huweza kufanana na dalili za ugonjwa mwingine. Kwa mfano, uchovu wa mwili na homa huweza kuwa dalili ya malaria na pia huweza kuwa dalili ya maambukizi ya njia ya mkojo, typhoid nk.
Sio vyema kutaka dawa fulani kwa ajili ya dalili fulani unayojisikia, bali ni vyema ukamueleza daktari au mtaalam wa afya jinsi unavyojisikia ili aweze kukushauri zaidi na kukusaidia.
Kupona vizuri kunaanzia na ugunduzi mzuri wa tatizo.
TUNAKUTAKIA AFYA NJEMA !!